Masaibu ya walevi na wake zao

25 Oct 2013

Kuna nyumba ya mlevi mmoja nje kuna shimo kubwa la maji bila mfuniko.

Siku moja karudi usiku kalewa tooooop, mambo yakawa hivi:

MUME: Fungua mlango!
MKE: Leo sifungui! Nimechoshwa na ulevi wako.

MUME: kama hufungui najitupa kwenye hili shimo nife kabisa.
MKE. Kufa huna faida yoyote duniani!.

MUME kachukua jiwe kubwa kalitupa kwenye shimo dubwi!
MKE kajifunga kanga, kafungua mlango. Ghafla mume kaingia ndani na kumfungia mke nje.

MKE: Nifungulie la sivyo nitapiga kelele majirani waje.
MUME: Piga kelele na wakija uwambie unakotoka wapi usiku huu na kanga moja.

JOIN GROUP KENYA


 

ADVERTISEMENTS