Where is the hatespeech? Full transcription of Sen. Muthama Johnstone speech at Uhuru park:
Wewe Rais, mshahara wako hakuna mtu anajua. Allowance zako hakuna mtu anajua. Pesa ambayo ilibebwa na Anne Waiguru kwa mfuko wake ni wewe tu unajua. Mimi nauliza, huyu Waiguru, kwani ni asali na ikaongezewa sukari?
Nitoboe nisitoboe? Nitoboe nisitoboe?
[Audience: TOBOAAAAAAAA!!]
Sisi hatutakaa kitako kuona Waiguru anabeba Millioni mia tisa na Uhuru anasimana na kusema Waiguru si mwizi.
Alafu anafukuza mama Ngilu kama mbwa sokoni, lakini huyu kipenzi cha moyo anaambiwa beba.
Nitoboe? Nitoboe? Nitoboe?
[Audience: TOBOAAAAAAA!!]
Uhuru anasema yakwamba, ati walimu wa Rwanda, Burundi and Uganda, wanalipwa zaidi ya walimu wetu. Kama Uhuru umena baada ya kuuza maziwa Uganda, na baada ya kusaidia Nkurunziza kubadilisha katiba kugandamiza waburundi, mimi nakwambia hii ni nchi tofauti kabisa!
Na tutakataa katakata kunyanyaswa na mtu yeyote. Uhuru umechukua ulipokuwa Rais, ulichukua Shillingi Billioni nane, ukasema ni za kuandikisha wakenya upya. Mshaona kipande mpya?
Ukachukua billioni ishirini na tisa, ukasema ni za laptops.
Wananchi mshaona laptops?
Wewe Rais, ukatoka bila kujali ukitabasamu bila kujali haki ya Wakenya, ukasema Anglo leasing iliiba 1.4 Billion shillings.
Wewe rais, ambaye huna heshima na mtu, ukachukua pesa zetu, Billioni mia mbili, ukaweka bond ya ulaya. Mshaona hizo pesa?
Wananchi sasa Uhuru kwasababu yeye alisema ile elimu alitaka, akapita mlango wa nyuma, akawekewa pesa, anataka nyinyi na watoto wenu wakose masomo ndio waendelee kuwa watumwa wa kulamba wale wengine matako yao. Mtakubali? Mtakubali watoto wenu walambe matako?
Kwahivo kama watoto wa maskini wako nyumbani, Uhuru ujue, you are not the president of the republic of Kenya. And you are not leading Kenyans.
Tunakutaka nyumbani, uende Gatundu, una nyumba ya kutosha, ukae huko na upeleke Anne Waiguru huko.
Nitoboe nisitoboe? Nitoboe nisitoboe?
[Audience: TOBOAAAAAAAA]
Tunajua pesa ulizoiba. Tunajua pesa zimeibiwa na wewe na Ruto. Mnatoa wapi kila wiki Millioni kumi ya kutoa katika harambee? na kabla hamjaenda ikulu, tulikuwa tunajua maisha yenu. Wacheni kutudanganya!
Where is Hatespeech?
Where did he disrespect women?
Where did he say anything about certain tribe?
By George Nyongesa
ALSO READ:
#IStandWithMuthama hashtag washes down Kenyan Twitter trends
TRENDING THIS WEEK
- Death toll in Garissa University terror strike hits 147
- Court nullyfies Jomo Kenyatta's order on beach plots
- Irregular land allocations from Kenyatta's regime now haunts Kenya
- Star newspaper van vandalized at a police station
- Lupita named worlds most beautiful woman
- What really matters in life - the real essence
- On evolution and creation - our Biology curriculum
- NgiluSinghJokes - Kenyan trends rock! Part 1
- Rogue police shoot at anti-corruption officers to escape bribery charge
- How they fixed Ruto to the ICC - VIDEO